Hatua moja muhimu ya kufanikiwa kibiashara

Siku zote Musa alikuwa kijana mwenye uchapa kazi kutoka Moshi mjini. Alikuwa na duka dogo la vifaa vya ujenzi — misumari, nondo, mabati, saruji na vifaa vingine vidogo. Tangu alipolianzisha, aliamini kwamba angeinuka haraka na kuwa mmoja wa wafanyabiashara wakubwa wa mji huo. Lakini miaka ikapita bila mafanikio aliyotarajia.

Kila siku Musa alilifungua duka alfajiri, akihakikisha kila bidhaa ipo sehemu yake. Wateja walipita, wengine waliuliza bei, lakini wengi walikwenda bila kununua. Mara nyingi alihesabu fedha jioni na kugundua hana faida yoyote. Wakati mwingine hata kulipa kodi au kuongeza mzigo ilimlazimu kukopa kwa rafiki au ndugu.…CONTINUE READING