Mtaa wa Githurai 45 ulijaa kicheko na mshangao baada ya kijana mmoja aliyefahamika kwa jina la ‘Kevo’ kunaswa akitekeleza wizi wa aina yake ndani ya kanisa la mtaa huo. Kevo, ambaye mara nyingi huonekana akiwa wa kwanza kufika kanisani na kukaa viti vya mbele akiwa amevaa suti iliyopauka, alinaswa akitumia mbinu ya kisayansi ya “gundi na kijiti” ili kuvua noti kutoka kwenye sanduku la sadaka.
Tukio hilo lilitokea wakati wa ibada ya asubuhi, pale mhasibu wa kanisa alipoanza kuhisi kuwa kiwango cha sadaka kimekuwa kikipungua kwa namna isiyo ya kawaida, licha ya waumini kuongezeka. Leo, mhasibu huyo aliamua kuchungulia kupitia tundu la pazia la ofisi yake inayotazama sanduku la sadaka wakati wa maombi ya mwisho. Alimuona Kevo akijifanya kusujudu kwa unyenyekevu karibu na sanduku hilo, lakini mkono wake ulikuwa ukishusha kijiti kirefu chenye gundi kali (super glue) kwenye ncha yake kupitia tundu la sanduku.…CONTINUE READING