Tukio la Ajabu: Mchungaji Avamiwa na Jeshi la Nyuki Akiwa Madhabahuni Akihubiri

Waumini wa kanisa moja huko maeneo ya Kakamega walibaki midomo wazi na kukimbia hovyo baada ya ibada ya Jumapili kugeuka kuwa uwanja wa vita, pale “jeshi” la nyuki lilipovamia kanisa hilo na kumshambulia mchungaji kiongozi peke yake, huku waumini wengine wakiachwa salama.

Tukio hilo la aina yake lilitokea majira ya saa tano asubuhi wakati mchungaji huyo (jina linahifadhiwa) akiwa katikati ya mahubiri mazito akilaani wizi na dhuluma. Ghafla, kundi kubwa la nyuki liliingia kanisani kupitia madirishani na kuelekea moja kwa moja mimbarani. Mchungaji alijaribu kufukuza nyuki hao kwa kutumia kitambaa chake na Biblia, lakini walimzunguka na kuanza kumshambulia sehemu mbalimbali za mwili.…CONTINUE READING